ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

WANANCHI  WAIOMBA THBUB  KUENDELEA  KUTOA ELIMU  YA HAKI  ZA BINADAMU  NA UTAWALA  MAENEO YA VIJIJI.

03 Jul, 2025
WANANCHI  WAIOMBA THBUB  KUENDELEA  KUTOA ELIMU  YA HAKI  ZA BINADAMU  NA UTAWALA  MAENEO YA VIJIJI.


Wananchi  wameiomba Tume ya Haki za Binadamu  na Utawala Bora Kutoa elimu ya haki za binadamu  na utawala bora katika maeneo ya vijijini ili waweze kujua haki zao.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Wananchi hao wamesema kuwa  watu wengi udhulumiwa haki zao  kutokana kuwa hawajui  mahala sahihi kupata haki zao pindiinapotokea imekiukwa.
"Unakutwa mtu amekamatwa bila kufuata utaratibu  tunaona sawa kwakua hatujui"amesema

Pia wananchi  hao wameishukuru kwakufika Maonesho ya Kimataifa  ya Biashara  ya Sabasaba ambapo imekua fursa kupata elimu hiyo