ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Wakazi wa Mwanza waaswa kutembelea Banda la THBUB kujipatia elimu ya haki za binadamu na utawala bora

27 Jan, 2025
Wakazi wa Mwanza waaswa kutembelea Banda la THBUB kujipatia elimu ya haki za binadamu na utawala bora

 Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza  Bw. Balandya Mayuganya baaada ya kutembelea banda la Ofisi za Tume za Haki za Binadamu na Utawala Bora na kujipatia elimu kuhusu haki za binadamu na misingi ya utawala bora,  amewataka wakazi wa mwanza na viunga vyake kufika kwenye banda hilo ili waweze kupata elimu hiyo na pia kuwasilisha malalamiko yao yanayohusu uvunjwaji wa haki za binadamu na misingi ya utawala bora.

Wito huo  ameutoa Januari 25, 2025 wakati alipotembelea banda  la THBUB  baada ya  uzinduzi wa Maonesho ya Wiki ya Sheria  yanayoendelea katika Viwanja vya Nyamagana Mjini Mwanza.

Elimu hiyo inatolewa na Watumishi wa  Ofisi ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ,Tawi la Mwanza wakiongozwa na Mfawidhi Bw. Goldian  Binamungu ikiwa na lengo  la kuwaelimisha wananchi juu ya haki zao na misingi ya utawala bora.

 Maonesho ya Wiki ya Sheria ya wiki ya sheria yamezinduliwa Januari 25, 2025 na yatatamatika Februari 1, 2025.