ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

MASWI AITAKA THBUB KUWA TAASISI YA MFANO

05 Feb, 2025
MASWI AITAKA THBUB KUWA TAASISI YA MFANO

Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Eliakim Maswi amewataka watumishi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kufanya kazi kwa kuzingatia  sheria za nchi, maadili na nidhamu ya kazi.

 Maswi ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano wa 23 wa  Baraza  la Wafanyakazi wa uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma leo  Februari 5, 2025 .

" kazi mliyonayo ni kuithibitishia Serikali kwamba mko tayari kutekeleza majukumu mliyopewa kwa mujibu wa sheria  na mnatakiwa kuwa mfano bora wa kuigwa kwa kuwa  taasisi inayolinda haki za binadamu na misingi ya utawala bora " amesisitiza Maswi

Awali akitoa neno la utangulizi,   Mwenyekiti wa Baraza hilo, Bw. Patience Ntwina amesema kuwa lengo la mkutano huo ni kupitia na kujadili taarifa za utekelezaji wa shughuli za Tume kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na 2024/2025 na na  mapendekezo ya mpango na bajeti ya mwaka 2025/2026.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi (TUGHE) tawi la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bw. Pontian Kitorobombo, kwa niaba ya Wajumbe wa baraza hilo amemshukuru Katibu Mkuu kwa kufungua Mkutano huo na kuahidi kuwa wajumbe watahakikisha wanaisaidia taasisi kuwa kwa kujadili masuala yenye kuleta tija kwa taasisi na watumishi