ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

THBUB YAENDELEA KUTOA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KWA WATENDAJI KATA

29 Jan, 2025
THBUB  YAENDELEA KUTOA ELIMU YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KWA WATENDAJI KATA

Ujumbe wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala (THBUB) ukiongozwa  na Makamu Mwenyekiti Mhe. Mohamed Khamis  Hamad,umetoa mafunzo  kwa Watendaji wa Kata kutoka Kata zilizopo katika  Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, leo Januari  27, 2025  katika Ukumbi wa Mikutano uliopo katika Ofisi za Halmashauri hiyo.

Aidha, Mafunzo hayo yamelenga kuwakumbusha Watendaji hao namna ya kuheshimu haki za binadamu na kuzingatia misingi ya utawala bora wakati utekelezaji wa majakumu yao ikiwemo kuwashirikisha wananchi katika masuala mbalimbali  yanayowahusu

Pia, Watendaji hao wamepata nafasi ya kuuliza maswali sambamba na kuelezea changamoto  wanazokutana nazo wakati wa kutekeleza majukumu yao ya kila siku