ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

Kamishna THBUB atoa taarifa kuhusu ukusanyaji wa Maoni Zanzibar

26 Jul, 2024
Kamishna THBUB atoa taarifa kuhusu ukusanyaji wa Maoni Zanzibar

WADAU mbalimbali wametakiwa kutoamaoni yao ili kusaidia uandaaji wa

mpangokazi wa kitaifa wa haki zabinadamu na biashara.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya Habari kuhusiana na zoezi la ukusanyaji wa maoni

hayo huko Rahaleo Mjinu Unguja Kamishna Tume ya haki za binaadamu na Utawala

Bora Tanzania Mhe.Khatib Mwinyichande alisema tume inatarajia kuendesha zoezi laukusanyaji wa maoni ya wadau kuanzia julai 29 hadi agosti 2mwaka 2024 ili kupata taarifa muhimuzitakazosaidia kupatikana mpango shirikishiwa tume hiyo.

Alifahamisha kuwa Serikali zote mbili zipokwenye Maandalizi ya Mpango kazi wa

kitaifa wa haki za binaadamu , hivyo wadauwana mchango mkubwa katika kufanikisha

upatikanaji wa mpango huo.

Alieleza kuwa zoezi hilo litawafikia wadauwa utalii, uchumi wa buluu na nishati katika

maeneo mbalimbali ya mikoa ya Zanzibarbaada ya kukamilika kwa zoezi kama hilo

Tanzaniabara .

Aidha alisema tume imepanga kuwafikiamamlaka ya uhifadhi na utekelezaji wa Mji

Mkongwe,kamisheni ya Utalii Zanzibar,umoja wa hoteli (HAZ), umoja wawawekezaji wa utalii(ZATI) , umoja wawaongoza utalii (ZATOGA),umoja wawaendesha utalii (ZATO),mamlaka yakukuza uwekezaji (ZIPA) pamoja na

Mamlaka za mapato Tanzania na Zanzibarndani ya Mkoa wa Mjini magharibi.

Vilevile alisema julai 31,2024 Tumeinatarajia kufanya mikutano na baadhi yawafanyakazi wa hoteli za kitalii zilizopoNungwi na Kendwa na wananchi wanaoishi

pembezoni mwa hoteli hizo pamoja nakuzungumza wananchi wanaoishi eneo la

uchimaji mchanga Donge Chechele ilikupata maoni yao.

Alifahamisha kuwa julai 29 ,2024 tume imepanga kukutana na wananchi wanaoishi

karibu na eneo la uchimbaji na uchakatajiwa matofali ya kifusi Vitongoji Mkoa wa

Kaskazini Pemba.Kamishna huyo aliwataja wadau wa uchumi

wa buluu wanaotarajiwa kufikiwa kuwa nipamoja na Mamlaka ya kusimamia Uvuvi

wa Bahari kuu, Shirika la Biashara laZanzibar (ZSTC) shirika lameli na bandari, kampuni ya mwani,wakulimana na wafanyabiashara wamwani,pamoja na wafanyabiashara wa

samaki katika maeneo mbali ya MjiniMagharibi, kusini unguja,kusini naKaskazini Pemba .

Hatahivyo alieleza kuwa zoezi hilolitafanyika kwa ushirikiano na wajumbe

walioteuliwa na Waziri wa Katiba na Sheriawa jamhuri ya Muungano wa Tanzania

kutoka katika taasisi za Serikali na binafsipamoja na asasi za kiraia kutoka Tanzania

bara na Zanzibar.

Tume ya haki za binaadamu na UtawalaBora (THBUB) ni chombo chenye jukumu la

kuhamasisha hifadhi ya haki za binaadamuna uzingatiwaji wa misingi ya Utawala Bora

kama majukumu yake yalivyoainshwakatika ibara 130(1)(a)-(h) ya katiba ya

Jamhuri ya muungano wa Tanzania 1977na sheria ya tume ya hakiza binaadamu na Utawala Bora Sura ya391 ya mwaka 2021 kifungu cha 6.