ADEM Logo
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA

Tunajenga utamaduni wa kuheshimu haki za binadamu, misingi ya utawala bora na utu wa mtu
ADEM Logo

JAMII IELIMISHWE UMUHIMU WA KUTUNZA NA KUHESHIMU UTU WA BINADAMU; M/KITI WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU

19 Jul, 2024
JAMII IELIMISHWE UMUHIMU WA KUTUNZA NA KUHESHIMU UTU WA BINADAMU; M/KITI WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU

TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Nchini,imetoa wito kwa Viongozi wa Siasa   Dini na Jamii kwa ujumla ,kuhusu kuelimisha jamii  umuhimu wakutunza na kuheshimu  utu wa  binadamu.

 Akiongea Ofisini kwake, Jijini Dodoma mbele ya waandishi wa vyombo mbalimbali vya Habari, Mwenyekiti wa Tume Mhe.Mathew Mwaimu (JajiMstaafu), amesema  kuwa kuna umuhimu wa viongozi hao kutoa elimu hiyo itakayosaidia kuondoa matukio ya mauaji ambayo yamekuwa yakitokea katika maeneo mbalimbali ya nchi.

 Jaji Mwaimu  ametoa mfano wa mauaji ya Mtoto mwenye  Ualbino, Asimwe Novart ambaye alichukuliwa nyumbani kwao Kamachumu Mkoani Kagera May 30, 2024 17,2024 akiwa ameuawa na kukatwa baadhi ya viungo vya mwili wake.

 “Viongozi wa dini na siasa wanajukumu kubwa la kutoa elimu   ambayo itasaidia jamii ijue umuhimu wa kutunza na kuheshimu  utu wa  binadamu wenzao”, amesema Mhe.Mwaimu

Ameongeza kuwa  Serikali ione umuhimu wa kuweka nguvu katika maeneo ya mipakani hasa mikoa ya kaskazini Magharibi ambako matukio kama hayo yamekuwa yakijitokeza kwa madai hayo ya Imani za kishirikina “ati viungo vya albino vinaweza kusababisha upatikanaji wa madini kwenye migodi na pia uongozi kwa wagombea wa kisiasa

 

 Aidha,Mhe. Mwaimu amebainisha kuwaTume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora,imekuwa ikipokea  malalamiko mengi   kuhusu migogoro ya Ardhi Nchini, ambapo Mkoa wa Dodoma ndio unaongoza na  changamoto kubwa  ikiwa  kutokuwepo kwa ushirikishwaji.

“Suala la mipango miji ni zuri katika uendelezaji wa miji hasa pale watu wa ardhi wanapokuwa wanafanya upimai ni vyema wakakaa na wananchi na kuwashirikisha ili kuondokana na migogoro hiyo”.Amesema Mhe.Mwaimu

 Katika hatua nyingine,Mhe Mwaimu amesema kuwa Tume pia imepokea  malalamiko ya watumishi wa Umma  katika upande wa ucheleweshwaji wa mafao kwa wastaafu,mapunjo ya mshahara pamoja na Kikokotoo.