The Commission for Human Rights and Good Governance (CHRAGG) is an independent government department, established as the national focal point institution for the promotion and protection of human rights and duties as well as good governance in Tanzania. CHRAGG was established under Article 129(1) of the Constitution of the United Republic of Tanzania of 1977 as amended by Act No. 3 of 2000.
The Commission became operational on the 1st July 2001 after the coming into force of the Commission the Human Rights and Good Governance Act No7 of 2001 as amended by Act No 16 of 2001 and Government Notice No. 311 of 8th June 2001. The Commission was officially inaugurated in March 2002 following the appointment of Commissioners by the President of the United Republic of Tanzania. download Act No. 7
MKUTANO UNAOZUNGUMZIA MASUALA YA UHURU NA USALAMA WA MTANDAO (STOCKHOLM INTERNET FORUM ON INTERNET FREEDOM FOR GLOBAL DEVELOPMENT – SIF13) UMEANZA LEO MJINI STOCKHOLM. MEI 22 – 23 2013
Mkutano wa Internet Forum unaendelea mjini Stockholm kwa siku ya pili, ukijadili mambo muhimu kama upatikanaji wa mtandao kwa watu wote na kwa gharama nafuu (Free access for all) na jinsi ya kuchochea maendeleo ya ubunifu na kutengeneza programu na vifaa vya TEHAMA (Accerelating innovations in ICT for transformative growth)ambayo wananchi wengi watakuwa wana uwezo wa kuvipata na kuvimiliki.

Waziri wa Ushirikiano wa Kimataifa wa sweden Bi. Gunilla Carlsson akifafanua jinsi gani Mtandao unaweza kutumika katika kuwaletea maemaendeleo wananchi
- Waziri wa Technologia ya Mawasiliano na Habari wa Sweden Bi. Anna-Karin Hatt, Professor Paula Uimonen, Director of SPIDER wakizungumza na Bw. Wilfred warioba, kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Dr. Jabiri Bakari CEO wa Tanzania e-Governance Tanzania.
TUME YATOA MADA KWA WAJUMBE WA BODI YA WAKURUGENZI YA “SWEDISH PROGRAME FOR ICT DEVELOPMENT IN REGIONS” KUHUSU MFUMO MPYA WA KOMPYUTA WA KUWASILISHA MALALAMIKO MBELE YA TUME KWA KUTUMIA UJUMBE WA SIMU YA KIGANJANI.MEI 21,2013
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imeweza kutoa mada kuhusu mfumo ambao imeianzisha wa kutumia ujumbe wa simu za kiganjani katika kupokea malalamiko yanayowasilishwa na wananchi mbele ya TUME. Mfumo huu ambao unatumia simu za kawaida, unawawezesha wananchi kutuma malalamiko yao ambayo yanafikia kwenye mfumo wa kielektroniki wa TUME ambapo wachunguzi wa TUME watakuwa wanashughulikia malalamiko yote yanayowasilishwa kama ambavyo inavyoshughulikia malalamiko yanayowasilishwa kwa njia nyingine mfano kuandika barua, au malalmiko yanayowasilishwa mbele ya Tume kwa njia ya kufika katika ofisi za TUME . Mfumo huu ni baadhi ya mikakati ya Tume katika kuhakikisha kuwa huduma zake zinawafikia wananchi wengi kwa urahisi na kwa wakati.

Bw.Wilfred Warioba Akitoa Mada kwa wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya SPIDER – Stockholm University kuhusiana na mfumo mpwa wa kielektroniki ambao unatumia simu ya kiganjani katika kuwasilisha malalamiko
SPIDER ni moja ya wafadhili ambao wanaisaidia TUME katika maeneo ya ICT ndio iliyosaidia kutengenezwa kwa mfumo huo. Bw. Warioba aliwasilisha mada hiyo makao makuu ya SPIDER ambayo yapo mjini Stockholm tarehe 21 Mei 2013.
MKUTANO UNAOZUNGUMZIA MASUALA YA UHURU NA USALAMA WA MTANDAO (STOCKHOLM INTERNET FORUM ON INTERNET FREEDOM FOR GLOBAL DEVELOPMENT – SIF13) UMEANZA LEO MJINI STOCKHOLM. MEI 22 – 23 2013
Mkutano unaozungumzia masuala ya uhuru na usalama wa mtandao kwa maendeleo ya Dunia umeaza leo mjini stockholm. Mkutano huo ambao umeandaliwa na Wizara ya mambo ya Nje ya Sweden umefunguliwa leo MEI 22, 2013 na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden Hon. Carl Bret. Mkutano huu muhimu ambao unakutanisha wataalamu wa masuala ya Internet na (policy makers) kutoka nchi zaidi ya Tisini na Tano(95) unazungumzia mambo muhimu kuhusiana na uhuru wa Mtandao ambao unahitaji kulindwa na kuheshimiwa na bila kusahau Usalama wa raia na maendeleo yao.
Mkutano huu wa siku mbili utazungumzia changamoto zilizopo ikiwa na ukweli kwamba kuna baadhi ya serikali za baadhi ya nchi duniani zimekuwa zikitaka kuwa na (control) na maamuzi makubwa kuhusiana na uhuru wa Mtandao(Internet) kwa sababu zao binafsi kwa kisingizio cha usalama au kulinda usalama wa raia.

Bw. Wilfred Warioba akiwa na Fadi Chehadé, na Raisi na CEO wa (Internet Corporation for Assigned Names and Numbers, ICANN)

From far right Dr.Jabir Bakari CEO of Tanzania e-Governance, Dr. Dorothy Okello form Makerere University and Founder of WOUGNET, Mr. Wilfred Warioba from Commission for Human Rights and Good Governance-Tanzania, Mr. John Ulanga, Executive Director, the Foundation for Civil Society - Tanzania

Bw. Warioba kutoka Tume ya haki za Binadamu na Utawala Bora, akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden Mhe. Carl Bildt.
Machapisho ya TUME
Pata vipeperushi mbalimbali vinavyotoa maelekezo kuhusu huduma na kazi za Tume zaidi..
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA WAZINDUA KITABU CHA KUONGEZA UELEWA WA WANANCHI KUHUSU WAJIBU NA HAKI ZAO NA MAJUKUMU YA POLISI
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tarehe 15.03.2013 imezindual kitabu cha “Mambo 101 unayohitaji kuyafahamu kuhusu polisi laki
ni unaogopa kuyauliza” kazi ya utayarishaji wa kitabu hicho umeandaliwa chini ya mradi wa kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu haki zao na kazi za polisi.
Uzinduzi wa kitabu hicho umefanyika Tarehe 15.03.2013 katika ukumbi wa mikutano wa Tume na mheshimiwa mgeni rasmi na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Angela Kairuki.
Mradi huu unatekelezwa kwa pamoja na Commonwealth Human Rights Initiative yenye makao yake jijini New Delhi nchini India kwa kushirikiana na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora ya Tanzania baada ya kutiliana saini mkataba wa maelewano hapo tarehe 15 Novemba, 2012.
Mradi huu unalenga kuongeza uelewa wa wananchi, na pia uelewa wa polisi kuhusu wajibu, kusudi, muundo, na haki za wananchi wanapokutana na polisi katika utekelezaji wa majukumu yao. soma habari zaidi, hotuba ya Naibu Waziri
Capacity-building Seminar on Accountability, Transparency and the Rule of Law
The Commission for Human Rights and Good Governance of Tanzania (CHRAGG) in collaboration with the International Ombudsman Institute (IOI) will conduct a capacity building seminar on Accountability, Transparency and Rule of Law for African region. The participants of the seminar will come from all English speaking African IOI member institutions. These are Botswana, Gambia, Ghana, Lesotho, Malawi, Mauritius, Namibia, Sierra Leone, South Africa, Sudan, Tanzania, Uganda, and Zambia. Each member institution will be represented by one participant. The seminar will be held in Dar es Salaam, Tanzania. IOI is the chief sponsor of the seminar. (IOI has agreed to grant EUR 7,500.00 [seven thousands five hundreds Euros] to CHRAGG for the implementation of the seminar). more..
WARSHA YA MASHIRIKIANO BAINA YA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA NA TAASISI YA OMBUSMAN YA DENMARK
Warsha ya siku mbili imefanyika katika ukumbi wa mikutano wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB). Warsha hii imefunguliwa na Mwenyekiti wa Tume Mhe. Jaji Mstaafu Amiri Ramadhani Manento. Warsha hii ina malengo ya kubadilishana uzoefu na utendaji wa Kazi ambazo zinashabihiana baina ya Taasisi hizi mbili
Mwenyekiti wa THBUB Mhe.Jaji kiongozi Mstaafu Amiri R. Manento akiongoza kikao cha ushirikiano kati ya Tume na Ombusman kutoka Denmark, kulia kwake ni Bw. Jens Olsen Mkurugenzi wa International Relations,kushoto ni Bi. Mary Massay Katibu Mtendaji wa Tume pamoja na viongozi wa ngazi za juu wa Tume
Pichani Bi.Mary Massay akimkaribisha Mwenyekiti wa Tume ili aweze kufungua na kuendesha kikao
Baadhi ya maofisa wa Tume wakifuatilia kwa karibu mazungumzo kwenye kikao,Maofisa wa ngazi za juu wa THBUB wakifuatilia kikao, mbele ktoka kulia ni Mkurugenzi wa Utafiti na Nyaraka Bi. Epiphania Mfundo, Kaimu mkurugenzi wa Elimu kwa Umma Bw. Alexander Sales, na Bw. Emanuel Barigila Afisa Mchunguzi
Viongozi wa juu wa THBUB wakifuatilia kikao, Bi Mahafoudha Amid Makamu mwenyekiti wa Tume, Kamishana Bi. Benadetha Gambishi na Bw. Kennedy Mchomvu
Mkuu wa Kitengo cha Kompyuta wa THBUB Bw. Wilfred Warioba, na Kaimu Mkurugenzi wa Utawala Bora Bi. Fatuma Muya wakibadilishana mawazo wakati wa mapumziko na Bw.Jens Olsen.
.
Afisa mchunguzi mkuu Bw.Vincent Mbombo na Jens Olsen na kaimu Mkurugenzi wa utawara bora Bi.Fatuma Muya wakibadilishana mawazo
Mkurugenzi wa Utafiti na Nyaraka Bibi Epiphania Mfundo akiwasilisha mada kwenye kikao
MAADHIMISHO YA SIKU YA HAKI ZA BINADAMU
10 December 2012
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe.Jaji kiongozi (mstaafu) Amiri R. Manento akihutubia siku ya Haki za Binadamu na Kuzuia na kupambana na Rushwa katika viwanja vya mnazi mmoja. mapema leo (picha na Mbaraka Kambona)
Mgeni Rasmi wa kilele cha Maadhimisho ya Haki za Binadamu na Kupambana na Kuzuia rushwa Mhe. Mizengo Pinda akipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha mifumo ya habari na mawasiliano ya kompyuta Bw. Wilfred Warioba katika Banda la Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kuhusu kazi za Tume na Mfumo mpya wa kuwasilisha malalamiko mbele ya Tume kwa kutumia ujumbe wa simu ya Kiganjani katika viwanja vya mnazi mmoja mapema leo (picha na Mbaraka Kambona)
Mgeni Rasmi wa kilele cha Maadhimisho ya Haki za Binadamu na Kupambana na Kuzuia rushwa Mhe. Mizengo Pinda na Makamu Mwenyekiti wa Tume Mhe. Mahfoudha Hamid wakipata maelezo kutoka kwa maofisa wa THBUB walipotembelea banda la TUME
Wageni mbali mbali wakipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha mifumo ya habari na mawasiliano ya kompyuta Bw. Wilfred Warioba katika banda la THBUB siku ya Maadhimisho ya Haki za Binadamu na Kupambana na Kuzuia rushwa yaliyofanyika katika viwanja vya mnazi mmoja mapema leo. (picha na Mbaraka Kambona - THBUB)
THBUB YAANDAA WARSHA YA TEHAMA NA MAENDELEO YA DEMOCRASIA NA HAKI ZA BINADAMU
Makamu mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu Mhe. Mahfoudha Alley Hamid
amefungua warsha ya Siku moja ya Wataalamu wa Taaluma ya Habari na mawasiliano na habari TEHAMA pamoja na wataalamu wa demokrasia na haki za binadamu , warsha hiyo umefanyika siku ya Jumanne Tarehe 4 Disemba 2012 katika ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora. Warsha hii itafuatiwa na Kongamano la kimataifa la siku mbili kuhusu masuala ya maendeleo ya demokrasia kwa kutumia TEHAMA ambalo linatarajiwa kufanyika Tarehe 5-6 Disemba 2012, Dar es Salaam. soma zaidi…, soma hotuba
MUHTASARI WA TAARIFA YA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA YA UCHUNGUZI WA TUKIO LILILOPELEKEA KIFO CHA DAUDI MWANGOSI KILICHOTOKEA SEPTEMBA 2, 2012 KIJIJINI NYOLOLO, WILAYA YA MUFINDI, MKOANI IRINGA
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ni idara huru ya serikali iliyoundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 129(1)(c) cha Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na Sheria ya Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Na. 7 ya mwaka 2001. Jukumu kubwa la Tume ni kulinda, kutetea na kuhifadhi haki za binadamu nchini. Katika kutekeleza jukumu hilo Tume imepewa mamlaka ya kupokea malalamiko (kwa njia mbalimbali) kutoka kwa mtu yeyote au kuanzisha uchunguzi wake yenyewe endapo itaona kuna uvunjifu wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora.
Kwa kuzingatia majukumu hayo, Tume ilianzisha uchunguzi wake yenyewe baada ya vyombo vya habari kutoa taarifa ya tukio la kifo cha Daudi Mwangosi. Tume iliunda timu ya watu watatu iliyoongozwa na Mhe. Kamishna Bernadeta Gambishi akisaidiwa na maafisa wawili, Bwana Gabriel Lubyagila na Bwana Yohana Mcharo. Timu hiyo ilifanya uchunguzi wake kuanzia tarehe 13-19 Septemba, 2012.
Katika uchunguzi uliofanywa, Tume ilizingatia zaidi masuala ya uvunjwaji wa haki za binadamu na ukiukwaji wa misingi ya utawala bora. Hivyo basi, Tume ilitilia maanani Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, sheria mbalimbali za nchi na mikataba ya kimataifa na ya kikanda inayohusu haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia. soma zaidi...
Massay stresses discipline in SHIMIWI games
THE Executive Secretary of the Commission for Human Rights and Good Governance (CHRAGG), Mrs. Mary Massay has urged Haki Sports Club players to maintain discipline
during the on-going inter-ministerial games, popularly known in its Kiswahili acronym as “SHIMIWI.”
Speaking at a farewell gathering held at CHRAGG offices, alongLuthuli Streetin the City recently, Mrs. Massay underscored the importance of discipline in sports, and told the players to uphold it at any cost during the competitions.
She also called upon players to work hard and ensure effective participation during the tournaments so as to emerge victorious in all the matches. read more….
Maafisa 21 wapata mafunzo ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro
Na Catherine Moshi (TUico)
TUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) kupitia Ofisi ya Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali watu, hivi karibuni ilitoa mafunzo ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro kwa maafisa uchunguzi 21 kutoka idara tano za Tume hiyo.
Mafunzo hayo ya siku mbili yaliyofanyika Agosti 13 – 14, 2012 makao makuu ya ofisi za Tume, mtaa wa Luthuli, Jijini Dar es Salaam yaliwahusisha Maafisa uchunguzi kutoka idara za Utawala Bora, Haki za Binadamu, Huduma za Kisheria, Elimu kwa Umma na Mafunzo na Idara ya Utafiti na Nyaraka.
Akifungua Mafunzo hayo, Kamishna wa THBUB, Mhe. Bernadeta Gambishi aliwaasa washiriki kuzingatia mafunzo hayo kutokana na umuhimu wake kwa kazi wazifanyazo kila siku ambazo zinahusisha masuala ya usuluhishi na utatuzi wa migogoro. Aidha, Mhe. Gambishi alionyesha furaha yake kwa kuanza kwa mafunzo hayo baada ya kuahirishwa mara kadhaa kutokana na sababu mbalimbali.
“Naelewa muda wa mafunzo haya ni mdogo ukilinganisha na mambo mnayotakiwa kujifunza; ila ni vizuri kuwa na umakini nayo kwa sababu yatatusaidia katika utendaji kazi wetu wa kila siku na kuwafanya muwe na lengo moja katika ufanyaji kazi wenu na kueneza elimu ambayo wawezeshaji wenu watawapa,” alisema.
Akiwakaribisha wawezeshaji wa mafunzo hayo, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Rasilimali watu ya Tume, Bibi Florida Kazora, alisema kuwa mafunzo hayo yatakuwa endelevu na yenye kuhusisha mada tofauti. Aidha, alieleza kuwa ofisi yake iko tayari kushirikiana na Idara nyingine katika kuandaa na kutoa mafunzo yatakayowajengea uwezo maafisa wa Tume katika kazi zao, na kwamba inakaribisha maoni kuhusiana na mafunzo yanayotolewa.
Mafunzo hayo yaliyoelezea njia za utatuzi wa migogoro mbalimbali na jinsi ya kufanya usuluhu wa migogoro katika jamii yaliongozwa na wawezeshaji wawili kutoka THBUB, Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utawala Bora, Bi. Fatuma Muya na Mkurugenzi wa Idara ya Haki za Binadamu, Bwana Francis Nzuki.
Mafunzo mengine ya jinsi hii yatafanyika pindi ofisi ya Mkurugenzi Utawala na Rasilimali watu itakapokuwa imeandaa mada na muda wa kuendesha mafunzo hayo.
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA
(THBUB)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
TAMKO LA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KULAANI KITENDO CHA KUPIGWA NA KUJERUHIWA KWA DK. STEPHEN ULIMBOKA KILICHOTOKEA HUKO MABWEPANDE, JIJINI DAR ES SALAAM USIKU WA TAREHE 26 JUNI, 2012
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imesikitishwa kwa kitendo alichofanyiwa Dk. Steven Ulimboka cha kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa vibaya na watu wasiojulikana kilichotokea tarehe 26 usiku, Juni 2012 na kukutwa ametupwa katika eneo la Mabwepande lililoko nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam. Soma taarifa zaidi..
RAISI AMWAPISHA KATIBU MTENDAJI WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KUWA KAMISHNA WA TUME YA USULUHISHI NA UAMUZI
Mheshimiwa Raisi Jakaya Mrisho Kikwete amemwapisha Katibu Mtendaji wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Bibi Mary Massay kuwa kamishna wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, hafla ya kumwapisha ilifanyika leo Ikulu dar es salaam.
Bibi Mary Massay ambaye ni katibu Mtendaji wa Tume atashikilia wadhifa huo ambao majukumu yake ni ya kushiriki katika vikao vya kufanya maamuzi ya Tume, kusimamia maamuzi ya Haki za binadamu na Utawala Bora Bibi Mary Massay ameteuliwa na kuapishwa kuwa kuwa Kamishna wa Tume ya usuluhishi na uamuzi kazi hiyo ambayo itakuwa ni (part time) soma habari zaidi..
KAMISHNA WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA ATEULIWA KUWA JAJI WA MAHAKAMA KUU YA TANZANIA
Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa

Mhe. Demello Jaji Mteule ambaye alikuwa ni Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Kamishna wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mhe. Joaquine De-Mello kuwa Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Mhe. Joaquine ni miongoni mwa Majaji 10 walioteuliwa na Mhe. Raisi hivi karibuni
Mheshimiwa De-mello anatarajiwa Kuapishwa siku ya Jumanne Tarehe 19.06.2012 kwenye viwanja vya Ikulu saa nne (4) asubuhi kushika wadhifa wake huo.
Ndani ya Tume Mhe .Demello amekuwa akifanya kazi kwenye za Ukamishna kwenye dawati la Wanawake na watoto. Tume inachukua fursa hii kumpongeza kwa uteuzi huo ingawa inakiri kuondokewa na Kamishna mchapakazi.
Ni matumaini ya Tume Mhe. Demello ataenda kuendeleza harakati za Kulinda na Kutetea haki za binadamu hususani haki za wanawake na watoto kwa uadilifu na weledi. Tume inampa pongezi kwa uteuzi huo na pia tunamtakia kila la kheri katika kazi yake mpya baada ya kuapishwa. soma zaidi…
TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA YAPOKEA MSAADA WA MAKTABA YA ELEKTRONIKI
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
imepokea Maktaba ya ki-elektronik (e-Granary Digital Library) kutoka taasisi ya kimataifa ya Kimarekani inayohudumia watu wenye ulemavu (United States International Council on Disability) kupitia Shirika la Misaada la Kimataifa (USAID) Tanzania.
Maktaba hizo mbili zimetolewa kwa ajili ya ofisi mbili za Tume, Dar es Salaam ambayo ni makao makuu ya Tume pamoja na Tawi la Mwanza.
soma habari zaidi…
CHRAGG REFRESHES JUDGES’ MEMORIES IN HUMAN RIGHTS
The Commission for Human Rights and Good Governance (CHRAGG) recently conducted training on Human Rights in the Administration of Justice which involved High Court Judges and Senior Resident Magistrates from Tanzania mainland and Zanzibar.
The training which took place in Bagamoyo from 4th – 6th June, 2012 aimed at familiarizing the judicial staff with the International and Regional Human Rights Standards as far as the administration of justice is concerned. The Office of the United Nations High Commissioner for Human Rights (OHCHR), Regional Office for East Africa based in Addis Ababa, Ethiopia provided the technical and financial support for this training.
The training was attended by the Judges of the High Court of Tanzania, the High Court of Zanzibar, Registrars of these two higher judicial organs and Resident Magistrates. read more….