In The Spotlight
Mwenyekiti wa Tume, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (kulia) akimkaribisha Kamishna Rose Macharia kutoka Kenya alipofanya ziara katika ofisi za tume jijini Dodoma Novemba 22, 2019.
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Job Ndugai akiongea na viongozi wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (hawapo pichani) walipotembelea ofisini kwake Wilayani Kongwa Novemba 19, 2019. Kulia ni Mwenyekiti wa Tume, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu na kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Kongwa , Deogratius Ndejembi.
More News
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu an Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mathew Pauwa Mhina Mwaimu akiongea na watumishi wa tume (hawapo pichani) katika hafla fupi iliyoandaliwa na Tume kuwakaribisha viongozi hao. Kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mheshimiwa Mohamed Khamis. Kushoto ni Kaimu Katibu Mtendaji wa Tume, Hajjat Fatuma Muya na Kamishna, Mheshimiwa Khatib Mwinyi Chande.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Mheshimiwa Jaji Mstaafu Mathew Pauwa Mhina Mwaimu (katikati-waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wateule wenzake. Kulia ni Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Mohamed Khamis Hamad, Kushoto ni Kaimu Katibu Mtendaji, Hajjat Fatuma Muya. Wengine waliosimama kutoka kushoto ni Mheshimiwa Nyanda Josiah Shuli, Mheshimiwa Khatib Mwinyi Chande, Mheshimiwa Thomas Masanja, Mheshimiwa Amina Talib Ali na Dkt. Fatma Rashid Khalfan.
Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Mipango kutoka Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Laurent Burilo akiongea na washiriki wa kikao kazi cha kujadili hali ya haki za binadamu na kuibua matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu kwenye makundi ya wanawake, watoto na watu wenye ulemavu kilichofanyika Mkoani Morogoro, Oktoba 24—25, 2019.
Mwakilishi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Josephine Lyengi akitoa mada katika kikao kazi cha kujadili hali halisi ya haki za binadamu nchini na kuibua matukio ambayo bado yanaonekana ni changamoto kubwa na kuyatengenezea mpango kazi wa kushughulikia. Kikao hicho kinafanyika Mkoani Morogoro kuanzia Oktoba 24—25, 2019.
Kama tunavyofahamu kuwa siku ya Jumapili Novemba 24, 2019 Watanzania kote nchini watafanya uchaguzi wa viongozi ngazi ya Serikali za Mitaa. Hatua hiyo ya uchaguzi imetanguliwa na uandikishaji wapiga kura, uteuzi wa wagombea na kampeni za wagombea, hatua ambazo zimetekelezwa kwa mafanikio makubwa.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeridhishwa na idadi ya watu waliojitokeza kujiandikisha kupiga kura. Idadi hiyo imeongezeka ukilinganisha na idadi ya watu waliojiandikisha katika uchaguzi kama huo uliofanyika mwaka 2014.Soma Zaidi
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imepokea taarifa zinazohusu askari polisi kuwapiga na kudhalilisha watu wenye ulemavu katika tukio lililotokea asubuhi ya Jun 16,2017,Mtaa wa Sokoine Jijini Dares Salaam.Soma zaidi
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imepata taarifa kupitia vyombo vya habari kuhusu uvamizi wa kituo cha Luninga na Radio cha Clouds Media Group, uliofanywa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, usiku wa tarehe 17, Machi mwaka huu, akiwa na askari wenye silaha.
Hotuba ya Mheshimiwa Bahame Tom Nyanduga, Mwenyekiti wa Tume katika siku ya kupinga mateso na ukatili dhidi ya wazee duniani, tarehe 15 Juni 2017, yaliyofanyika katika ofisi za Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jengo la Haki, Dar es Salaam. Pakua hotuba kamili
Hotuba ya Mhe. Bahame Tom Nyanduga, Mwenyekiti wa Tume wakati wa hafla ya utoaji tuzo za umahiri wa uandishi wa habari tanzania (EJAT) 2015, ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam, aprili 29, 2016. Pakua hotuba kamili
Hotuba ya mwenyekiti wa Tume Mhe. Bahame T. Nyanduga, katika ufunguzi wa mkutano wa wadau kuhusu mikakati ya kukomesha mauaji na ukatili dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi , tarehe 18 Machi 2015 katika ofisi za Tume. Pakua hotuba kamili
Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu, Zanzibar, Omary Othman Makungu (katika) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa THBUB, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu(kulia kwake) na Viongozi wengine wa tume. Mwenyekiti wa tume alimtembelea Jaji Mkuu ofisini kwake Desemba 2, 2019.
Jaji Mkuu wa Mahakama Kuu, Visiwani Zanzibar, Omary Othman Makungu amemueleza Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu kuwa wako tayari kushirikiana tume kutatua kero za wananchi zinazohusu upatikanaji wa haki nchini.
Jaji Makungu alisema hayo alipokutana na Mwenyekiti wa tume ofisini kwake Visiwani Zanzibar Desemba 2, 2019.
Mwenyekiti wa THBUB Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akiongea katika kikao kilichofanyika Desemba 2, 2019 katika ofisi za Baraza la Wawakilishi. Kulia ni Spika wa Baraza la Wawakilishi Visiwani Zanzibar, Zubeir Ali Maulid.
Spika wa Baraza la Wawakilishi Visiwani Zanzibar, Zubeir Ali Maulid amemueleza Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu kuwa kazi aliyopewa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ni kubwa na ngumu.
Spika Maulid alieleza hayo katika kikao kilichofanyika kwenye ofisi za Baraza la wawakilishi mapema leo (Desemba 2, 2019) alipotembelewa na Mwenyekiti huyo.
Mwenyekiti wa (THBUB), Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu akiongea na wafanyakazi wa tume pamoja na wageni wengine waliohudhuria hafla fupi.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu ametembelea ofisi za taasisi hiyo zilizopo visiwani Zanzibar, ikiwa mara yake ya kwanza tangu alipokabidhiwa dhamana hiyo Novemba 4, 2019.
MAONI YA WANANCHI KUHUSU WAOMBAJI WANAOITWA KWENYE USAILI KWA AJILI YA NAFASI ZA MWENYEKITI, MAKAMU MWENYEKITI NA MAKAMISHNA WA TUME
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) ni taasisi huru ya umma na inayojitegemea iliyoanzishwa chini ya Ibara ya 129(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sura ya Pili ya Sheria yenye majukumu ya kuhakikisha kuwa haki za binadamu na utawala zinakuzwa, kulindwa na kuheshimiwa nchini
Kamati ya Uteuzi inawaalika raia wa Tanzania wenye sifa zinazotakiwa kuwasilisha maombi kwa nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Makamishna ili kujaza nafasi zilizo wazi katika Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora.Pakua Habari kamili . Read more
TUNAPENDA KUWATANGAZIA WADAU NA WATEJA WOTE WA TUME YA HAKI ZA BINADAMU NA UTAWALA BORA KWAMBA OFISI ZETU ZILIZOPO JENGO LA TANCOT ZIMEHAMIA JENGO LA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA MTAA WA MKWEPU. HIVYO HUDUMA ZOTE ZITATOLEWA HUKO KUANZIA TAREHE 01 JANUARI, 2019
UTAWALA